KAMA ulidhani winga wa zamani wa Yanga, Andrey Coutinho, amepotea kwenye ramani ya soka, baada ya kutemwa na wanajangwani hao, utakuwa umekosea, kwani Mbrazil huyo anaendelea kung’ara huko aliko.

Winga huyo anayekipiga Ligi ya Brazil ya Myanmir katika Klabu ya Rakhine United, kutokana na uwezo wake  wameamua kumpa unahodha na sasa  ni kiongozi wa wachezaji wenzake uwanjani.

Bahati mbaya klabu hiyo haijafanya vizuri msimu uliopita, kwani ilinusurika kushuka  daraja, iliyoshika nafasi ya 10  inayoshiriki timu 12.

Katika ligi hiyo, timu mbili za mwisho zinazoshuka daraja ambapo kikosi hicho cha akina Coutinho kiliponea tundu la sindano, baada ya Southern Myanmar waliomaliza wakiwa na pointi 14, huku Horizon wakiburuza mkia kwa  pointi saba kushuka.

Winga huyo aliwahi kucheza Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara akiwa na Yanga  ambaye aliletwa na aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Marcio Maximo.

Maximo alitimuliwa na Yanga baada ya kufungwa mabao 2-0 na Simba katika mchezo wa kirafiki wa Nani Mtani Jembe, uliochezwa Desemba 13 mwaka juzi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na nafasi yake kuchukuliwa na Hans  van der Pluijm.

Source-Bingwa

Post a Comment

 
Top