Uongozi wa Simba umefanikiwa kumuongezea  mkataba wa miaka miawili na nusu beki wake Mohamed Husein (Zimbwe jr) 

Simba imefanikiwa kushinda vita kubwa na kufanikiwa kumbakisha mlinzi huyo wa kushoto ambae amekuwa na misimu bora kwa miaka yote miwili aloitumikia Simba

Zimbwe amekuwa akigombaniwa na timu nyingi na baadhi ya vyombo kumpigia chapuo kwenda timu wanazozipenda wao mapema leo amesaini kandarasi ya miaka miwili na nusu kuendelea kuitumikia Simba mbele ya Rais wa Klabu hiyo Evance Aveva

Post a Comment

 
Top