Klabu
inayoshiriki ligi kuu uingereza, Swansea City (ya Wales), imemfuta kazi
aliyekuwa mkufunzi wa klabu hiyo, mtaliano, Francesco Guidolin, na kumwajiri
kwa muda kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Marekani Kasikazini, Bob Bradley.
Guidolin ambaye alikuwa akisheherekea siku yake ya kuzaliwa (zaliko), alifutwa
kazi tarehe 3 Oktoba, (siku ya Jumatatu), baada ya kufungwa 2-1 na Liverpool siku ya
Jumamosi. Swansea imeshinda mechi moja
tu ya kufungua ligi kati ya saba ilizocheza msimu huu. Licha ya kuiokoa
timu hiyo kutoshuka daraja, mkufunzi huyo aliandikiwa barua ya kukatishwa kandarasi yake, leo Jumatatu. Mkufunzi huyo alijiunga na klabu hiyo Januari mwaka huu kwa kandarasi
(contract) ya miaka miwili.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment