Ilishuhudiwa juzi (Jumapili) Real Madrid ikitoka vichwa chini uwanjani baada ya kutoka suluhu  ya 1-1 na timu ndogo (underdog) ya Eibar. Kwa matokeo hayo, R. Madrid imepata sare katika michezo minne mfululizo.  Kwa mujibu wa mchambuzi wa mpira, Guillem Balague, R. Madrid inacheza katika kiwango kibovu. Aidha, amemshutumu Zidane kama ndio chanzo cha timu hiyo kufanya vibaya. Pengine, amempa lawama mkufunzi wa Barcelona, Enrique kwa kukubali kipigo cha 4-3 kutoka kwa Celta Vigo siku ya Jumapili.

Balague hakubaliani na maneno ya Zidane kuwa sababu ya matokea mabovu ya michezo minne ya hivi karibuni, ni kukosekana kwa viungo wawili majeruhi Casemiro na Mondric. Anadai kuwa kukosekana kwa wachezaji wawili haimaanishi ufungwe na timu ndogo kama Eibar. Isitoshe, uwanjani, wachezaji wa R. Madrid wameonesha viwango vya chini, na pia, timu haioneshi ufundi wowote uwanjani na haiujui inafanya nini. Hii inatia mashaka mafunzo (training) wanayopata wachezaji kutoka kwa kocha wao.

Kwa upande wa mahasimu wao, A. Madridi wameendelea kutaka baada ya kuwafunga Valencia 2-0 na kuwahakikishia kuongoza msimamo wa ligi.


Ronaldo shows his frustration during the draw with EibarImage result for zidane

Post a Comment

 
Top