Leo katika Matini,
tunakuletea maelezo machache lakini yasiyo na upujufu kuhusiana na dini
mashuhuri yenye wafuasi wengi duniani, Buddha.
Budha, kwa
upande wake, bado haifahamiki kindakindaki katika jamii za Kiafrika, hii ni kwa
sababu haijaonelea kuathiri mioyo ya watu wengi kama zilivyo dini zilizotajwa
hapo awali. Neno “Budha” linatokana na jina la Gautama Buddha. Gautama (563
KK-483 BK) ndiye mwasisi na nembo ya kwanza ya dini ya Budha. Gautama alizaliwa
kwenye familia ya Siddhartha katika jiji la Nepal, kusini mwa Asia ya Zamani.
Baba yake alikuwa mfalme aliyetwa Suddodana Tharu na mamaye mlimbwende
aliyeitwa Mayadevi.
Inadaiwa
kuwa kipindi cha uzao wake, Gautama alitabiriwa na mnajimu wa mfalme (baba yake)
kuwa Mfalme Mkuu (the Great King), na iwapo angeondoka katika ufalme wake, basi
alitakikakana kuwa kiongozi hodari wa dini. Unajimu huu haukumfurahisha babaye ambaye
hakutaka mwanawe awe kiongozi wa dini.
Gautama
alipofikia utuuzima na kuelimika vema, alitambua jawabu thabiti la masumbuko/mateso
na namna ya kuukabili na kuudhibiti. Jawabu hilo aliliita Four Noble of Truths―suffering (why people unhappy), origin/source,
ends (the end of suffering) and marga/means to end the suferring―. Hata hivyo,
hakuwa na hakika iwapo atafundisha udhanivu wake huo mpya. Alijiuliza nafsini
mwake iwapo ulimwengu utakuwa tayari kupata mafundisho ya namna hii. Lakini mwishowe, aliamua kusafiri kwenda
mjini kuitwapo Sarnath kuwafunza watu
njia aliyoimaizi. Alifundisha watu njia hiyo (the eightfold path―the path to
the end of suffering), na watu walimakinika kumsikiliza.
Alipokuwa
akifundisha, hakujifanyiza kuwa yeye ama ni Mungu na/au hata kuwa mjumbe wa
Mungu. Alijitabanaisha kuwa yeye angali binadamu anayetafuta maana ya maisha
(enlightenment). Maishaye yote, alitembea kupita mji wa Nepali na sehemu za
India akihudumu akihubiria kile alichokuwa akikiamini, na kwamba kila mtu
anaweza kutafuta maana ya maisha. Aidha, alianzisha kundi lililoitwa Sangha liliomini katika mafundisho yake.
Kwa kweli tupu, watu waliwerevuka kupitia yeye. Na alipofikisha umri wa kipimo
cha miaka themanini aliiaga dunia kwa kile kilichodaiwa kuwa alikula chakula
chenye sumu (food poison).
Kwa hivi
sasa, tangu enzi yake hadi leo, mafundisho ya Gautama Buddha hujulikana kama Buddhism. Buddhism ni namna tu ya
kudondoa hisia za maumivu makali ambayo
watu wanahisi ndani ya safu ya mitima yao. Kwa mujibu wa Gautama Buddha,
maumivu/mateso ni sehemu ya maisha. Na kwamba, maumivu husababishwa hasa na
mrundikano na mshinikizo wa tamaa kali.
Mafundisho
ya Buddha yanasisitiza kuwa njia ya kuondoa tamaa na maumivu ni kufanya vitu
vyema, kuacha vitu viovu na kufunza akili/ufahamu wa mtu/watu. Aidha, Buddha
alifundisha watu kuwa na uwazo/utafakuri yakinifu (meditation), kufikiri kwa
kina wakiwa wamekaa kisanskriti.
Pengine
haijathibitika, ulimwengu wa ki-Buddha haujasema iwapo Mungu yupo au la. Bali,
aghalabu Buddha alifundisha kwamba watu hawapaswi kumtazamia Mungu pekee kutatua
mambo yao isipokuwa wao wenyewe. Hii itawezekana pale tu watu wakijifahamu
wenyewe (self enlightenment).
Hivi leo,
Ubuddha umesambaa sana Asia ambapo mafundisho makuu ni kuhakikisha watu
wakiishi katika maisha tulivu na kutawaliwa na ukweli/wema. Maisha tulivu
huashiriwa na amani na furaha.
Ni wazi
kuwa mafundisho ya Buddha ni murua na yana umuhimu hasa ulimwenguni, na kwamba
kila binadamu ana haja ya kupata mafundisho hayo muhimu.
Kwa
kufuatilia zaidi mafundisho na undani wa Buddha usiache kupitia vyanzo
vifuatavyo:
http//www.britannica.com/EBchecked/topic/1224840.2010
http//.buddhanet.net/e-learning/Buddhism/disciples
13.2010.


Post a Comment